Kifo cha muhammad ali kimezua malumbano makali katika ulingo wa kisiasa miongoni mwa wagombea wa kiti cha uraisi katika uchaguzi mkuu,utakaofanyika mwezi novemba nchini marekani.
Katika risala zake za rambirambi mgombea wa kiti cha urais kwa tiketi ya chama cha Republican Donald trump,amesema kuwa Ali kwa hakika alikuwa bingwa ambaye atakumbukwa na wengi mwaka jana ,Ali alilaani wito uliotolewa na bwana trump ya kuwazuia kabisa waislamu kuingia nchini marekani.
Kwa upande wake mgombea wa kiti cha urais kwa tiketi ya
chama cha Democratic Senetor Bernie sanders amemshutumu Bwana trump na kumtaja kuwa mnafiki.
Naye bi Hillary clinton amesema kuwa bwana trump anafaa kuhukumiwa kwa matamshi yake anayotoa.
Bondia huyo alifariki siku ya ijumaa huko Arizona,na alikuwa akiugua maradhi ya kusahau sahau,kwa zaidi ya mwaka 30.
Jumanne, 7 Juni 2016
RC AAGIZA MKURUGENZI HANANG AFIKISHA MAHAKAMANI
Mkuu wa mkoa manyara dr Joel bendera ameagiza aliyekuwa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Hanang,Felix mabula na aliyekuwa muweka hazina wa halmashauri hiyo Matonya mzengo wafikishwe mahakamani kujibu mashtaka ya upotevu wa sh 932 milioni.
Akuzungumza juzi wilayani Hanang Dr Bendera alisema taarifa ya uchunguzi wa tuhuma za ubadhirifu wa fedha ziliokuwa zinawakabili Mabula na Mizengo waliosimamishwa tangu april 6 mwaka,zimewaingiza hatianiani.
Dr Bendera alisema kamati hiyo ilibaini kuwa Mabula na Matonya wameisababishia halmashauri hiyo madeni ikiwemo hospitali ya wilaya(Tumaini) inayodaiwa na bohari ya dawa(MSD) sh34.606 milioni,hivyo wamepoteza sifa za utumishi wamefikishwa mahakamani.
POLISI WATAKA USHIRIKIANO KUTHIBITI UHALIFU MWANZA
Kamanda wa polisi wa mkoa wa mwanza Ahmed msangi amesema vyombo vya dola pekee haviwezi kupigana vita dhidi ya uhalifu bila ya kuwepo ushirikiano na wadau wengine.
Msangi alisema hayo wakati chama cha waandishi wa habari wa kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya na uhalifu Tanzania (ojadaet),kilipokuwa kinazindua kampeni ya kupinga vitendo hivyo.
"Amani,utulivu ni bidhaa adimu,tushirikiane kuona mkoa wetu unakuwa salama,maana hata uwekezaji hawezi kuwekeza katika sehemu ambayo siyo salama,hivyo kuendelea kutokea uhalifu ni kuwaogopesha,na kukwamisha maendeleo".alisema msangi
Msangi alisema hayo wakati chama cha waandishi wa habari wa kupiga vita matumizi ya dawa za kulevya na uhalifu Tanzania (ojadaet),kilipokuwa kinazindua kampeni ya kupinga vitendo hivyo.
"Amani,utulivu ni bidhaa adimu,tushirikiane kuona mkoa wetu unakuwa salama,maana hata uwekezaji hawezi kuwekeza katika sehemu ambayo siyo salama,hivyo kuendelea kutokea uhalifu ni kuwaogopesha,na kukwamisha maendeleo".alisema msangi
AUAWA KWA KUPORA SIMU
Mtu mmoja ameuawa kwa kipigo cha kuchomwa moto kwa tuhuma ya kupora simu ya mkononi aina ys tecno.
Kamanda wa polisi mkoa wa mwanza Ahmed msangi alisema juni 2 mtu huyo ambaye jina halikupatikana anaekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 25 hadi 35,aliuawa baada ya kumpora simu mpitanjia eneo la Ngaza kata ya Nyegezi jijini hapo.
"Kabla ya kupora simu,mtu aliyejulikana kwa jina la Aanica rwezaura alitishiwa na yule aliyeuawa kwa panga lakini wananchi wenye hasira kali walimwandama,kumpiga na hatimaye kumchoma moto hadi kufa".alisema kamanda msangi
Kamanda wa polisi mkoa wa mwanza Ahmed msangi alisema juni 2 mtu huyo ambaye jina halikupatikana anaekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 25 hadi 35,aliuawa baada ya kumpora simu mpitanjia eneo la Ngaza kata ya Nyegezi jijini hapo.
"Kabla ya kupora simu,mtu aliyejulikana kwa jina la Aanica rwezaura alitishiwa na yule aliyeuawa kwa panga lakini wananchi wenye hasira kali walimwandama,kumpiga na hatimaye kumchoma moto hadi kufa".alisema kamanda msangi
WANAFUNZI 130 WA CHUO KIKUU CHA TUMAINI TAWI LA MBEYA KUTOFANYA MTIHANI WA MWISHO KWA KUKOSA USAJILI WA NACTE
Zaidi ya wanafunzi 130 wanaosoma kozi ya afya ya jamii katika chuo kikuu cha Tumaini mikumira tawi la mbeya wako hatarini kutofanya mitihani yao ya mwisho baada ya uongozi wa chuo hicho kushindwa kukamilisha taratibu za kuwasajili kwa wakati kwenye baraza la taifa la elimu ya ufundi,NACTE.
Wanafunzi wa chuo kikuu cha Tumaini makumira tawi la mbeya ambao wamebakiza mwezi mmoja kuhitimu elimu yao ya chuoni hapo,wamekusanyika mbele ya majengo ya utawala wa chuo hicho na kupaza sauti zao wakitaka kujua hatma yao kuhusu usajili wao katika baraza la taifa la elimu ya ufundi,NACTE.
Kutokana na kutokuwa na uhakika wa kuhitimu elimu yao kwa amani,wanafunzi hao wamesikitishwa na uongozi wa chuo hicho kinachomilikiwa na kanisa kwa vitendo wanavyifanyiwa,hivyo wakaiomba serikali kuingia kati ili waweze kutendewa haki.
Wanafunzi wa chuo kikuu cha Tumaini makumira tawi la mbeya ambao wamebakiza mwezi mmoja kuhitimu elimu yao ya chuoni hapo,wamekusanyika mbele ya majengo ya utawala wa chuo hicho na kupaza sauti zao wakitaka kujua hatma yao kuhusu usajili wao katika baraza la taifa la elimu ya ufundi,NACTE.
Kutokana na kutokuwa na uhakika wa kuhitimu elimu yao kwa amani,wanafunzi hao wamesikitishwa na uongozi wa chuo hicho kinachomilikiwa na kanisa kwa vitendo wanavyifanyiwa,hivyo wakaiomba serikali kuingia kati ili waweze kutendewa haki.
BAADHI WAACHIWA TUHUMA ZA MAUAJI MSIKITINI
Kamanda wa polisi mkoani Mwanza Ahmed msangi amesema pamoja na kuwaachia watu ambao hakutaja idadi yao,bado wanafuatulia wengine ambao wanaonekana kuhusika na tukio hilo,bila kutaja idadi ya watu walioachiwa.
"Wapo baadhi walioachiwa,wengine watafikishwa mahakamani wakati wowote baada ya kuona ushahidi una kila aina ya dalili za kuhusika na tukio hilo".amesema msangi
Katika mauaji hayo,watu watatu waliuawa kwa kukatwa mapanga wakisali msikitini akiwemo imamu wa msikiti huo,Feruz ismail na wengine wawili na kumjeruhi mtoto wa miaka 13.
"Wapo baadhi walioachiwa,wengine watafikishwa mahakamani wakati wowote baada ya kuona ushahidi una kila aina ya dalili za kuhusika na tukio hilo".amesema msangi
Katika mauaji hayo,watu watatu waliuawa kwa kukatwa mapanga wakisali msikitini akiwemo imamu wa msikiti huo,Feruz ismail na wengine wawili na kumjeruhi mtoto wa miaka 13.
DIAMOND PLATINUMZ AFUNGUKA HAYA KUHUSU WEMA SEPETU
Diamond platinumz alisema haya kwenye kipindi cha FNL amesema kitendo akichofanya Wema kupost kazi zake anadhani imefika wakati labda Wema Sepetu ameona hakuna sababu ya yeye kuendelea kumchukia Diamond platinumz na ndiyo maana ameonyesha upendo kwa kusapoti kazi zake na za wasanii kutoka kwenye lebo yake.
"Kuna wakati inafika watu mnakuwa mmekuwa labda,mtu anaona hana sababu ya kuendelea kukuchukia au kuwa na vita na wewe,sababu mwanzo mkiwa bado mnaenda mnaona kuna vitu mko navyo ndiyo maana kuna kuwa na chuki kubwa,lakini ikifika wakati kila mtu amesonga mbele na maisha yake,ameridhika na naisha yake anaona kwanini nimuwekee vita mtu fulani hivyo anadhani labda wakati huo ndiyo huu maana mwenyewe nimeona kweli amepost
BET,amepost promo ya Rich mavoko kwangu mimi nafurahi kwasababu naona haina faida kwa sisi wasanii kuwekeana vita". alisema Diamond
Mbali na hilo Diamond platinumz alidai toka ameachana na Wema sepetu hana namba yake ya simu,hajawahi hata siku moja kumpigia simu wala Wema sepetu hajawahi kumpigia simu Diamond platinumz.
"Kuna wakati inafika watu mnakuwa mmekuwa labda,mtu anaona hana sababu ya kuendelea kukuchukia au kuwa na vita na wewe,sababu mwanzo mkiwa bado mnaenda mnaona kuna vitu mko navyo ndiyo maana kuna kuwa na chuki kubwa,lakini ikifika wakati kila mtu amesonga mbele na maisha yake,ameridhika na naisha yake anaona kwanini nimuwekee vita mtu fulani hivyo anadhani labda wakati huo ndiyo huu maana mwenyewe nimeona kweli amepost
BET,amepost promo ya Rich mavoko kwangu mimi nafurahi kwasababu naona haina faida kwa sisi wasanii kuwekeana vita". alisema Diamond
Mbali na hilo Diamond platinumz alidai toka ameachana na Wema sepetu hana namba yake ya simu,hajawahi hata siku moja kumpigia simu wala Wema sepetu hajawahi kumpigia simu Diamond platinumz.
ACT -Wazalendo YAUNGANA NA UKAWA KUFANYA MIKUTANO YA HADHARA
Chama cha siasa cha ACT-wazalendo nchini Tanzania kimesema kuwa kinakusudia mikutano ya hadhara katika miji mikubwa nchini kwa kushirikiana na vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA,kuongea na wananchi juu ya wabunge waliotolewa nje ya bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Tamko hilo limetolewa jana jijini Dar- es-salam na katibu mwenezi wa chama cha ACT-wazalendo Sabini Richard wakati akiongea na waandishi w habari jijini Dar-es-salaam juu ya hatua iliyochukuliwa na chama hicho kufuatia kutoridhishwa na mwenendo wa bunge kidemokrasia.
Mikutano hiyo inatarajiwa kuanzia jijini Dar-es-salaam na baadae kuelekea sehemu mbali mbali katika miji mimgine mikubwa nchini Tanzania.
Tamko hilo limetolewa jana jijini Dar- es-salam na katibu mwenezi wa chama cha ACT-wazalendo Sabini Richard wakati akiongea na waandishi w habari jijini Dar-es-salaam juu ya hatua iliyochukuliwa na chama hicho kufuatia kutoridhishwa na mwenendo wa bunge kidemokrasia.
Mikutano hiyo inatarajiwa kuanzia jijini Dar-es-salaam na baadae kuelekea sehemu mbali mbali katika miji mimgine mikubwa nchini Tanzania.
SAKATA LA SUKARI LAMALIZIKA WIKI HII- NTIBENDA
Mkuu wa mkoa wa Arusha Felix Ntibenda amesema kuanzia wiki ijayo tatizo la sukari litakuwa historia,kwani viwanda vya sukari vya ndani vinaanza uzalishaji,Ntibenda alisema hayo wakati akikabidhi mradi wa ufugaji kuku wa kienyeji na mbuzi wa maziwa katika kata ya Muriel eneo la kwa mrombo unaoendeshwa na mfuko wa maendeleo ya jamii( TASAF).
"Hivi sasa wananchi mnauziwa sukari kilo moja kwa shilingi 2,500 hadi 3,500 kwa kilo moja,lakini sasa tunasema sukari itapatikana kuanzia wiki ijayo na wanaofunga Ramadhan wasiwe na shaka,watapata sukari".alisema
Meya wa jiji la Arusha,Calist Lazaro amesema anaungana na serikali kuhakikisha maendeleo ya jiji la Arusha yatapatikana ikiwemo ukusanyaji wa bodi za majengo.
"Hivi sasa wananchi mnauziwa sukari kilo moja kwa shilingi 2,500 hadi 3,500 kwa kilo moja,lakini sasa tunasema sukari itapatikana kuanzia wiki ijayo na wanaofunga Ramadhan wasiwe na shaka,watapata sukari".alisema
Meya wa jiji la Arusha,Calist Lazaro amesema anaungana na serikali kuhakikisha maendeleo ya jiji la Arusha yatapatikana ikiwemo ukusanyaji wa bodi za majengo.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)