Kamanda wa polisi mkoani Mwanza Ahmed msangi amesema pamoja na kuwaachia watu ambao hakutaja idadi yao,bado wanafuatulia wengine ambao wanaonekana kuhusika na tukio hilo,bila kutaja idadi ya watu walioachiwa.
"Wapo baadhi walioachiwa,wengine watafikishwa mahakamani wakati wowote baada ya kuona ushahidi una kila aina ya dalili za kuhusika na tukio hilo".amesema msangi
Katika mauaji hayo,watu watatu waliuawa kwa kukatwa mapanga wakisali msikitini akiwemo imamu wa msikiti huo,Feruz ismail na wengine wawili na kumjeruhi mtoto wa miaka 13.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni