Jumanne, 7 Juni 2016

AUAWA KWA KUPORA SIMU

Mtu mmoja ameuawa kwa kipigo cha kuchomwa moto kwa tuhuma ya kupora simu ya mkononi aina ys tecno.


Kamanda wa polisi mkoa wa mwanza Ahmed msangi alisema juni 2 mtu huyo ambaye jina halikupatikana anaekadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka 25 hadi 35,aliuawa baada ya kumpora simu mpitanjia eneo la Ngaza kata ya Nyegezi jijini hapo.


"Kabla ya kupora simu,mtu aliyejulikana kwa jina la Aanica rwezaura alitishiwa na yule aliyeuawa kwa panga lakini wananchi wenye hasira kali walimwandama,kumpiga na hatimaye kumchoma moto hadi kufa".alisema kamanda msangi

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni